UKWELI TIBA.

Friday, January 13, 2006

bhalezee

bhalezee
Niko Kasulu.Kasulu kuna mambo yaani ajabu kwangu kwani sikuweza ona kabla ya mwaka huu.
Tarehe 1 ya januari ya mwaka 2006 usiku nilipata mwaliko wa kwenda kwenye pati moja maridadi sana.Unashangaa nini ?kusema maridadi sana! hata kasulu kuna pati maridadi sana.
Jamaa mmoja alikuja na kudumu cha lita kama siyo tatu basi mbili na wengine kama watano kwakiwa na chupa tupa za plastiki nao wakaingia.
Kweli kulikuwa na vinywaji na chakula cha kutosha....nilichoona sikutegemea hasa kwa wahiji wa watendaji.
Kwanza nilimwona jamaa mmoja akimimina soda ndani ya ile cupa tupu ya plastiki .Nikashikwa na shauku ya kutaka jua je?na wale wengine nao ndio matumizi yao?
Nikainuka na kumtafuta yule mwenye lita pili au sio mbili.... ah ah ah yeye nikamwona kwa macho weupi akiweka lita zake ndani ya mfuko huku ikiwa imejaa kama sio mvinyo basi maji ya bia ....Nikashindwa vumilia nika mtafuta mwenyeji wangu kulikoni kuhusiana jambo hili...cha ajabu hakushangaa kabisa ila akanimbia mbona ni jambo la kawaida sana.
Nikasogeza keyboard na..
Waelezee(BHALEZEE)

No comments: