UKWELI TIBA.

Monday, January 30, 2006

Rudi! Rudi Mwanangu Rudi!

RUDI!RUDI MWANANGU RUDI!

Rudi nyumbani mwanangu rudi
Rudi nyumbani pombe yakutosha rudi
Rudi Ukimwi hakuna Rudi
Rudi ! Rudi Mwanangu Rudi

Usifikirie Vinginevyo
Mimi Mzaziyo naomba rudi
Nakupenda Mwanangu Rudi
Rudi! Rudi Mwanangu Rudi

Swali Mwanangu jibu
Hivi ulipata hivyo na ukakosa vyote
Umepata kitu gani?
Rudi!Rudi Mwanangu Rudi

Najua wajua elimu unayo
najua wasema ulimwengu ni wako
Lakini wewe ni Dunia?
Rudi! Rudi Mwanamgu Rudi

Mwanangu watofautisha visa
Dhambi wasema makosa
Kisa eti makosa hukumu ni papo
Rudi! Rudi Mwanamgu Rudi

Dhambi eti ni Hukumu mpaka Mungu
Acha basi uishi pasi kujificha ficha
Rafiki zako mpaka uwe nazo?
Rudi! Rudi Mwanamgu Rudi

Nakupenda mwanangu nakupenda sana
Ugenini wapata taabu sana
Waishi kama kima;wafanya kazi kama punda aliyekodiwa
Rudi! Rudi Mwanamgu Rudi

Kisa kwa kuvaa nguo za kisasa na kuwa na...
Na usalama wako je?si ardhini au angani
Popote waweza kupata ajali
Rudi! Rudi Mwanamgu Rudi

Najua wanikumbuka Mwanagu
Najua wanipenda Mwanangu
Lakini kwa nini unakaa kimya
Rudi! Rudi Mwanamgu Rudi

Kwa nini Mwanangu......?
Mwanangu......
Itikia basi Mwanangu.....
Rudi! Rudi Mwanamgu Rudi

Mwanangu.......Africa


nilikwenda bize

SAMAHANINI
Kwani nini nasema hivyo?naomba msamaha kwa kutokuwa nanyi tangia wiki moja hivi iliyopita pasi mawasilano nanyi.Huwa tuna sameheana sisi wa Wana wa Adamu.Ahsante sana.
Nikwenda bizeyaani shughuli zangu za kila siku ilifikia mahali amabpo sukiweza kufanya zote kwa mudawangu wa kawaida;kiasi ambacho hata muda wa mimi kuweza kuandika ninacho fikiri kuwa mdogo sana.Niliweza kufikiri ila kitendo hicho kilikwenda sambamba na kitendo kufanyika....aha aha ndipo nikajua nini hasa maana ya kwenda au kuwa bize.

Kama kawaida niliweza kuhudhuria burudani kadhaa hasa mashindano ya kombe la mataifa ya Africa(Tanzania wakiwa kama Watazamaji wakuu wa mashindano hayo)...Ndio mbona washangaa? Ndio kama watazamaji wakuu wa mashindano hayo kwani Taifa Stars?iko Huko? Naomba jina ilibadilishwe.....sababu ninazo tena nyingi sana sio mimi tu hata wewe moja ni neno taifa Stars..Kwani Kufikiri na kutendo kwao tofauti kabisa.

Wako Bize! na nini?

Wednesday, January 18, 2006

Dar mpaka Kigoma

FIKIRI:
Unaweza kujaribu kufikiri jambo mpaka ikafikia mahali ukajiona wewe kweli una akil sana. AH AHA lakini cha kusitajabisha pinde watu wanapojua kuwa unachofikiri waanza ulizana kweli jamaa yuko timamu?

Dar Mpaka Kigoma ni safari yangu mimi nilioianza 2003 mwezi wa 8 na tarehe 5 stesheni ya Gari moshi(treni) ya Jijini Dar es salaam.Ni masimulizi yatayojili kila siku kwako Mungu akiendelea kuwa nami katika dunia hii.

Masimulizi yatakuja yakiwa na matukio ya kweli kuanzia siku ya kwanza kuondoka nyumbani Dar-mpka kufika Kigoma hasa wilyani Kasulu.Kwa watu ambao nitawataja kwa majina naomba msamaha kwa hilo hasa tukio tukio utapolitafasili vinginevyo.Naomba ujue hii dunia matukio yote si ya kweli nikiwa na maana kwamba kwani hayana mwisho.Pia kwa sentensi iliyotangulia maomba usilete ubishi.

Najua kila mtu ana akili timamu(kufuatana na sikolojia ya Maendeleo ya Mwana wa adamu) akilelewa vizuri kabisa kabla ya tendo na baada ya tendo(......).

SAFARI YAANZA

))001:NDANI YA TEKSI KUELEKEA STESHENI-dreva ANTHONY
NUKUU:Mtu huchoka zaidi anapokuwa hana kabisa cha kufanya.
ANTHONYna msikani vuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu aaaaaaaaaaahhhhhhhhhhhhhhh mara Mwanga anawanga na gari bila ubishi lakata kona na kupaki pembeni ya barabara.....Mwanga anasogelea gari na swali moja baada la lingine....Mara kijana Leseni yako iko wapi?...Kijana Bima yako mbona chakavu sana....imekwisha muda nini?...najiuliza kwani haisomeki !nashindwa sema kwanibado dakika 45 tu kwa ya muda wa kulipoti stesheni fika.....HASIRA ZA MNYONGE! kelele zake....!! Afande basi kijana atakuona akinifikisha stesheni..hakuna taabu!

Afande(Mwanga)alikubali kwani tulikuwa mita chache kutoka stesheni

Tuesday, January 17, 2006

Jana?

Jana Bwana!Kila mara utasikia mtu anasema kuhusiana na jana yake;Yaani jana yake yeye aliweza fanya nini au alishindwa fanya nini hapa chini ya jua.

Kila mara watu wengi hupenda sana jana yao na wengi pia uchukia jana yao.Inafikia hata wakati wengi huondoa uhai wao kwa sababu ya jana.Huwa najaribu sana kufikiria kuhusu jana yangu......naogopa sana kuwa JIZI(Mwendawazimu)...naona jana yangu ilikuwa nzuri sana lakini nani?nani?aliweza haribu jana yangu? Bila shaka si mimi hata hivyo nashindwa sema nani kwa jana yangu ila kama sio mwanasiasa basi ni wewe kiongozi wa dini au jamii....Unakataa ni wewe !Ndio wewe eh ehe unakataa nini?Wewe ndio unashindwa kukemea jambo mbaya ninapotokee mbele yako,Wewe unashindwa fanya jambo zuri kila siku...ndio unayanfa baadhi ya watu wanaokupenda walie kwa mambo yako.....
jana?jana yako umewafanya au hata imeweza haribu kabisa matumaini yangu...hata yako ya kuwa fulani....Jana yako inakufanya hata shuhuli unayofanya usiipende sana...
Naipenda sana jana yangu..ndio kama wewe unavyoipenda jana yako....jana yako imekufanya Jamii ikupende Ongera sana jana yako ndio inayokupa chakula ccvha kila siku na jamii yako.....

Jana yako inakufuata popote pale uendapo hata kama utajificha jamii yako inapokutafuta jana yako .Mpaka ndani ya .....Kaburi yako kwa heshima kubwa huku ukiacha Jamii yako inayokupenda na kukuenzi ukuharibu kwakukatili mkubwa jana yao.
Jana ?....

Sunday, January 15, 2006

bhalezee

Kigoma Weather


--------------------------------------------------------------------------------
at: 9:00 pm EAT F° C°

Currently:
22°

Partly Cloudy High: 26°

Low: 20°





· Text Forecast
· Get Yahoo! Weather on your desktop


5 Day Forecast

Today Tomorrow Tue Wed Thu 6-10 Day



Scattered Thunderstorms


High: 26°
Low: 20°


Scattered Thunderstorms


High: 25°
Low: 20°


Showers


High: 23°
Low: 19°


Scattered Thunderstorms


High: 25°
Low: 18°


Scattered Thunderstorms


High: 26°
Low: 18°
Extended Forecast

Harusi ya jana

HARUSI YA JANA
Jana nilialikwa harusini.Ongera sana maharusi na wote tuliouzulia harusi .
Kulichanganya sana kinywaji:kulikuwa na Coca cola,fanta nyeupe kama ziitavyo,nyeusi,passion,Sprite,tangawizi na nyingine nyingi.
ambacho kilikuwa kigeni kwangu kwenye harusi hiyo ni dada mmoja ambaya ndani ya muda wa masaa matatu ya sherehe hiyo aliweza kunywa soda 13.
Nasema kitu kigeni kwani sikuwahi ona kabla jambo hilo na huku akiwa na shauku ya kuendelea kunywa lakini bahati nzuri baada ya kula chakula kasi yake ya kuendelea kunywa ilipungua sana.Mimi nikaondoka .
Habari zilizojiri baadaye zilisema mpaka mwisho wa sherehe aliweza kunywa soda 23.
Harusi ya jana

Friday, January 13, 2006

bhalezee

bhalezee
Niko Kasulu.Kasulu kuna mambo yaani ajabu kwangu kwani sikuweza ona kabla ya mwaka huu.
Tarehe 1 ya januari ya mwaka 2006 usiku nilipata mwaliko wa kwenda kwenye pati moja maridadi sana.Unashangaa nini ?kusema maridadi sana! hata kasulu kuna pati maridadi sana.
Jamaa mmoja alikuja na kudumu cha lita kama siyo tatu basi mbili na wengine kama watano kwakiwa na chupa tupa za plastiki nao wakaingia.
Kweli kulikuwa na vinywaji na chakula cha kutosha....nilichoona sikutegemea hasa kwa wahiji wa watendaji.
Kwanza nilimwona jamaa mmoja akimimina soda ndani ya ile cupa tupu ya plastiki .Nikashikwa na shauku ya kutaka jua je?na wale wengine nao ndio matumizi yao?
Nikainuka na kumtafuta yule mwenye lita pili au sio mbili.... ah ah ah yeye nikamwona kwa macho weupi akiweka lita zake ndani ya mfuko huku ikiwa imejaa kama sio mvinyo basi maji ya bia ....Nikashindwa vumilia nika mtafuta mwenyeji wangu kulikoni kuhusiana jambo hili...cha ajabu hakushangaa kabisa ila akanimbia mbona ni jambo la kawaida sana.
Nikasogeza keyboard na..
Waelezee(BHALEZEE)

bhalezee

Sema!unatakiwa husema nini hasa kinachokusibu!Usipo sema nani atajua wewe una tatizo au upedezewi na jambo unalofanyiwa ni mbaya kwako.Sema(waelezee-bhalezee) wajua ni jambo mbaya sana kwako......
Sema kwa vitendo yaani onesha waziwazi kwamba unachosema au unavyosema unamaanaisha hivyo kweli.
Sio ooH oH unajua mimi sitaki jambo hili huku haoneshi kabisa kwa vitendo kwamaba jambo hilo linakukera sana.
BHALEZEE