UKWELI TIBA.

Monday, October 09, 2006

UTATA?

UTATA?
Safari ya kutoka Kasulu mjini kuelekea Dar es salaam yaanza kupitia Kigoma Mjini kwa usafiri wa Basi,Treni,Basi na Teksi.

Kasulu kwapanda ndani ya basi na kusubiri Wasafiri wengine kwa muda wa masaa wawili kamili kisha gari laanza safari.Polisi ambaye kwa jina maarufu anaitwa Trafiki anatukamata mita 20 tu kutoka kituo cha mabasi hayo na kudai waziwazi chake(RUSHWA).

Gari kwa kweli alisitahili hata kidogo kuwemo barabarani......kuanzia bodi yake na mwishoni mwa safari na gundua hata dreva wake naye hastahili kuwemo ndani ya chombo hicho........NAAMBIWA MUDA WA GENERETA KUPUMZIKA UMEFIKA Baadaye.......

Monday, October 02, 2006

UWEZO NINAO?


Uwezo ninao?Ni swali ambalo kila siku kwangu ni ngumu sana kulijibu,kiasi ambacho naomba msaada kwenu ndugu zangu popote mlipo.Na bila shaka waza jiuliza uwezo gani hasa nataka pata msaada wa ndugu nisaidi.Si pesa au mali naomba nisaidieni.
Naipenda sana Tanzania......hilo ni la kwanza,Pili;nawapenda sana viongozi wetu wa Mtanzania,Tatu;Uwezo wangu wa kujua wapi Tanzania Tunakwenda(Mtarajio ya kisera)
Naipenda sana Tanzania;siwezi kuikimbia nchi yangu nzuri sana Tanzania.Tanzania ooh Tanzania ooh .....Una Maziwa ya maji yenye samaki ambao sisi hatuwezi kuvua kwa nguvu zetu ila uwezo wa kununua Mashingingi ya bei mbaya kwa kila kiongozi wa KAYA.....Sitawataja kwa majina yao( UWEZO NINAO?).


Ardhi yako Tanzania Ooh Tanzania ina madini mengi;ambayo hatuwezi kuyajimbua kama sio kuyajimba......Hata kufanya mikataba kuhusiana na madini hatuwezi.(UWEZO NINAO?)Najiuliza....Naomba jibu...Pengine sishibi ndio sababu ya kushindwa jibu swali hili.
PILI:Nawapenda sana viongozi wetu woooooooooooooooooote.Nawapenda kiasi ambacho sijui yupi ni mkweli....Kwangu ni kwamba wanaposema ni ukweli mtupu.....Mfano;HAKI SAWA,NI TAWAJAZA MAPESA,MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA NA SUALA LA UMEME(Na sio tatizo)SI MUDA LA MREFU:Nukuu ya Kiongozi wangu mpendwa wa nchi aha aha HAKUNA MTU ANAYEKULA SAMAKI WABOVU(MAPANKI).............

TATU:Matajio ya Kisera;KASI MPYA,ARI MPYA NA NGUVU MPYA.(UWEZO NINAO?)Nashindwa jua kama sera inaendana na vitu gani hasa?KASI MPYA.....kwenda wapi?ARI MPYA baaday ya hamasa gani hasa?NGUVU MPYA baada ya kula nini hasa?au baadaya kuwekewa mazingira gani ya msingi......Sio ujuzi wa sera.UWEZO NINAO? naomba msaada najua ndugu zangu ni wema kwani mtoto wangu akiuliza niweze kumjibu kwa ufasaha.