UKWELI TIBA.

Wednesday, December 20, 2006

NI SEHEMU TU YA KIGOMA PICHANI

Ni mwisho wa reli.Ni msemo ambao niliusikia takribani miaka zaidi ya Ishirini(20) na ushee tangia niishi hapa Tanzania;ndio hapa Tanzania?! na sio Tanganyika iliyotimizi miaka 45 ya Uhuru wake toka chini ya makucha?Tunamiriki maliasili zote sisi wewe?
Kuanzia Mara mpaka Mtwara ukipitia njia zote za lami majira yote ya mwaka.

Ndio Tanzania Bara?Watoto wake wanajua Uvinza kuna chumvi,Mikumi,Serengerti na Bonde la Moyowosi kuna wanyama pori na Gombe kuna Sokwe mtu.......Lakini atafikaje? kwani kutoka Tanzania mpaka Kigoma ni siku si chini ya tatu?

Mazingira yake yanachomwa sana kwa moto na acha hukataji wa mti.Niko huku sasa ni mwaka wa tatu nimeshaambiwa si na mtu mmoja ...........una ona ule mlima pale.....ule kule kuliko na msitu na wanyama pori kibao(wengi sana).

Wakimbizi walipoingia..............mafuta ya taa yaliporipuka bei...na sio kupanda;kwani zaidi ya asilimia 97 ya wenyeji wanatumia kuni?

No comments: