UKWELI TIBA.

Tuesday, February 07, 2006

SISI NI WAVIVU?

Kweli sisi ni wavivu? Yaani sisi Watanzania.Inawezekana kweli kwani mpaka sasa bajeti ya nchi yetu inatoka ng'ambo.Kila kitu tunacho...ardhini,majini na hata watu wapo(tupo).

Kuna rafiki yangu anajibu swali hili kwa kusema walioko madarakani tangia unaoitwa Uhuru ni mwezi na walafi na wanalaghai na waongo.Wegina yeye anasema wote si viongozi wema!kama wapo wachache sana.Na damu yetu iwe juu yao.

Ni wavivu! kutokana na hoja hizo mbili kwani hakuna hata miongoni mwetu sisi yaani wenye nchi anaonesha kukerwa kweli kweli na jambo hilo la kuishi maisha duni na yasiyo na matarajio kwa familia yako(zetu).

Hakuna hata maandamano hata milio ya makelele...hakuna hata risasi za amani yaani maneno ya kweli kama risasi pindi yatokapo mpata yule anayeambiwa hayo maneno ajue kweli kweli hasipo sikie yatamjeruhi au kuua kabisa(INDIA inawezekana kwanini kwetu tusiweze?)

Tuamua sasa wakati ukifika hakuna hatayekuwa salama hata kama ukifa yawezekana maiti yako isizikwe ndan ya kaburi.

Eti Sisi tunaongea sana?



SISI kweli ni wavivu

Friday, February 03, 2006

MIMI SENEGAL

Mimi Senegal bwana....!Mimi DRC Congo na mimi ni......

Hayo ni baadhi ya maneno ya watazamaji(Watanzania).Ndio sisi ni watazamaji wa kudumu wa mashindano yeyote yale hapa duniani.

Sisi ni watazamaji na sisi sio Watanzania katika jambo la kushangilia na kushabikia mashindano hapa duniani.Usikatae kabisa hata wewe kama sio Manchester basi ni Liverpool kama Mimi....Mimi ni Liverpool!MIMI NI LIVERPOOL!

Kwenye utandawizi ndio Utandawazi (kama Tafsida) ukweli ni utandawazi kila mtu (hana) haki ya kupenda apendacho mradi kwake ni kizuri....Kwenye utandawazi hata Wabunge kujiongezea mishahara yao Ruksa kabisa....Unabisha nini?1

Hata Serikali kutoa ahadi ruksa hata ukibisha haisaidiee kitu.....Mimi Liverpool Fan( hapa mshangiliaji)......ETAENDELEA

Thursday, February 02, 2006

NINGE...

jana sio juzi!Ninge....Kamwe hakui kabisa.Maisha yako ukiyafananisha na ya fulani ;basi wewe sio wewe ila ni yeye.Hivyo basi hufai kuishi.Hapana Fulani mwenyewe hasiwe Yule ambaye jamii haimuhitaji kuwa naye!ISIWE FULANI KUWA WEWE!

Wednesday, February 01, 2006

Tutapona?

Mungu najua yote! Nadhani kwangu ndio jibu sahihi kwa swali linaloulizwa na watu kwa sasa kila siku kutokana na balaa la njaa linalonyemea taifa late ua tusema ambalo linaliandama taifa letu.

Hapa Kasulu mvua zinanyesha karibu kila siku lakini sikiwa zimechelewa sana;na zinanyesha kwa namna ya ajabu sana....yaajabu sana kwani ndani ya wilaya hii ya Kasulu kuna sehemu mvua haijanyesha kwa wiki sasa na mahindi ambayo yalichelewa kupandwa yaanza kukauka,Kweli Tutapona?

Maajabu mengi!Wilaya ya kasulu inarutuba ya kutosha sana lakini ardhi ilimwayo ni nadhani hata robo ya hiyo yenye rutuba ndio ilimwayo...Kwani jembe bado ni la mkono kwenye ardhi ngumu sana na Wilaya nzima ina trekta moja tu (nimeambiwa sijawahi liona likilima)
Kasulu inaongoza kwa mkoa wa Kigoma kulima mazao ya chakula (ajabu) Haina hata hatua mbili ya barabara ya lami au ya kutumika majira yote.

Ajabulingine kelele:Kwangu naweza sema ndio Wilaya yenye kelele kuliko zote kwa hapa Bongoland(Tanzania).Kwani kila upitapo vichochoro vya Kasulu kuna Jenereta au kajenereta kama wenyeji wasemavyo kila kitu weka mwanzo neno (ka) linaunguruma na kuachia moshi mchafu sana.
Wenyeji wana sema ukija umeme tutakuwa nchini na sisi.....Nina hakika hawana taarifa za gharama za umeme wa TANESCO ziendazo kasi kama....taja wewe!

Sahamani rafiki yangu Philipo! yeye uamini ongezeko la watuhasa kwenye famila yao ni kutokana na kukosekana kwa umeme na barabara bora.Ni kweli?Malizia---------------------

Tutapona kweli? hakuna miundo mbinu Tata.....kweli akili zetu na hata kwenye mazingira yetu.Kwani kila kijana anafikiria kutoka na kila mwenye Usiasa anafikiria kuwa fulani kwenye sehemu fulani hata kwa Uchawi(nimekosa neno ...sahihi)Ila sijui wewe wataka kutokaje.....
Kuana rafiki yangu Kule KAHAMA uamini kwamba nchii hii kila mtu akipewa anachotaka mambo yatakuwa safi.....Wape bangi watakao....Kwani unadhani wanaongoza hawajui wapi inatoka......Wape Wazinzi.....Wape Rushwa.....Nawe?